190. SIKU NILIPOKUWA DHAMBINI
Siku nilipokuwa dhambini, Nikaambiwa juu ya Mwokozi; Nikasikiliza na furaha, Kufahamu kwamba nitaokoka. Niliambiwa Yesu apenda, Aliyenifia Msalaba; Dhambi zangu ataziondoa, Nikaambiwa Yesu apenda. Tangu nilipoonja upendo, Yesu hukaa ndani ya moyo; Humu dunia ni kama mbingu, Kwani Kumjua Mwokozi ni tamu. Ili kazi nimfanyie Bwana; Maneno hayo ninayataja, Ninatembea pamoja naye, Hapo ndipo furaha siku zote.