204.BWANA WANGU YU MCHUNGAJI


Bwana wangu yu mchungaji,

Hunilaza chini;

Kwa malisho ya majani

Huniongoza mimi.


Nafsi yangu huhuisha,

Ananitembeza

Njiani mwake kwa haki yake,

Katika jina lake.


Nijapopita bondeni

Mwisho mwa maisha,

Sitaogopa baya lo lote,

Wewe upo na mimi.


Wema wako na fadhili,

Itanifuata

Katika nyumba yake Mungu,

Kutakuwa makao.

Comments

Popular posts from this blog

193. KATIKA YESU SINA SHAKA

197. MUNGU ALIAHIDI