193. KATIKA YESU SINA SHAKA



Katika Yesu sina shaka,

Yeye amenitosha;

Pendo lake lanipendeza,

Kwake nina ushirika.


Katika Yesu sina shaka,

Amenilinda po pote;

Kwangu Neno lake limetimizwa,

Kwake sina shaka lo lote.


Katika Yesu sina shaka,

Ingawa nina haja;

Hunifariji na upendo,

Ajua kufurahisha.


Kaitka Yesu sina shaka,

Na ameniridhisha;

Yeye tayari kuniponya,

Kwake nimefadhilika.

Comments

Popular posts from this blog

197. MUNGU ALIAHIDI