197. MUNGU ALIAHIDI



Mungu aliahidi,

Na kwa fadhili yake;

Tutapata pumziko,

Katika mkono wake.


    Tukiona mashaka mengi,

    "Tulia", amri yake,

    Roho yangu ina amani,

    Katika mkono wake


Ijapo hufahamu,

Na usifadhaike;

Hutasumbuka tena,

Katika mkono wake.


Na ukishughulika,

Kwa mambo siku zote;

Roho itapumzika,

Katika mkono wake.


Furaha ya ajabu,

Tena amani yake;

Zimewekwa tayari

Katika mkono wake.

Comments

Popular posts from this blog

193. KATIKA YESU SINA SHAKA