203. NIKILEMEWA NA MIZIGO MINGI



Nikilemewa na mizigo mingi,

Nikitembea bila tumaini;

Mwokozi wangu ameniahidi,

Niambie ahadi zake tena.


    Niimbie ahadi tena,

    Mara kwa mara ahadi tena;

    Na nitafurahi, hapana huzuni,

    Niambie ahadi zake tena.


Nikizungukwa na hatari nyingi,

Na nikishikwa na hofu moyoni;

"Sitakuacha," asema Mwokozi,

Niambie ahadi zake tena.


Na nikiingia mbinguni kwake,

Kupumzika salamani milele;

Ahadi zake tamu, zikumbukwe,

Niambie ahadi zake tena.

Comments

Popular posts from this blog

193. KATIKA YESU SINA SHAKA

197. MUNGU ALIAHIDI