198. MUNGU BABA YANGU, U MWAMINIFU



Mungu Baba yangu, U Mwaminifu,

Hakuna geuzo ndani yako;

Hubadiliki, wewe ndiwe sawa,

Jana, leo na siku zijazo.


    Wewe Mwaminifu, Wewe Mwaminifu,

    Kila siku fadhili napewa;

    Vitu vyote ninavyo umenipa

    Wewe Mwaminifu kwangu Bwana.


Na viumbe vyote hulingamana,

Kuonyesha utukufu wako;

Jua, na mvua, mwezi tena nyota

Hulishuhudia pendo lako.


Samaha la dhambi, tena amani,

Hivi vyote ni baraka zako;

Nguvu zako zitadumu milele,

Nimebarikiwa sasa kwako.

Comments

Popular posts from this blog

193. KATIKA YESU SINA SHAKA

197. MUNGU ALIAHIDI