190. SIKU NILIPOKUWA DHAMBINI



Siku nilipokuwa dhambini,

Nikaambiwa juu ya Mwokozi;

Nikasikiliza na furaha,

Kufahamu kwamba nitaokoka.


    Niliambiwa Yesu apenda,

    Aliyenifia Msalaba;

    Dhambi zangu ataziondoa,

    Nikaambiwa Yesu apenda.


Tangu nilipoonja upendo,

Yesu hukaa ndani ya moyo;

Humu dunia ni kama mbingu,

Kwani Kumjua Mwokozi ni tamu.


Ili kazi nimfanyie Bwana;

Maneno hayo ninayataja,

Ninatembea pamoja naye,

Hapo ndipo furaha siku zote.

Comments

Popular posts from this blog

193. KATIKA YESU SINA SHAKA

197. MUNGU ALIAHIDI