211. KATIKA GETHSEMANE YESU ALITESWA


Katika Gethsemane Yesu aliteswa,

Kikombe chenye huzuni, hapo alikunywa;

Pa Kalvari, Msalabani aliuchukua,

Alitenda mapenzi ya Baba.


Pekee, ndiyo pekee, Yesu alikufa,

Pekee, ndiyo pekee alinifungua;

Dunia hii iliaibishwa hata Yesu

Alitenda mapenzi ya Baba.


Yesu alikubali kunifia mtini,

Akamwaga damu yake nisife dhambini;

Akawekwa katika kabirini mwambani,

Alitenda mapenzi ya Baba.


Alifufuka kutoka kifo na kaburi,

Akawa Mshindi juu ya mauti na dhambi;

Akaniokoa nisiende hukumuni,

Alitenda mapenzi ya Baba.

Comments

Popular posts from this blog

193. KATIKA YESU SINA SHAKA

197. MUNGU ALIAHIDI